Tunalala kwenye vumbi na matope ili wewe ulale kitandani,
Tunala na bunduki ili wewe ulale na mwenzi wako,
Tunalala porini ili wewe ulale kwenye nyumba,
Unavaa kofia maridadi ya kupendeza, sisi tunavaa kofia ngumu na nzito za chuma,
Unavaa "vest" nzuri ya pamba, sisi tunavaa "vest" za shaba,
Unavaa mkanda wa ngozi kiunoni, sisi tunavaa mikanda ya risasi,
Asubuhi unaamshwa na "alarm" nzuri ya simu yako, sisi tunaamshwa na milio ya mabomu na risasi,
Unatembelea gari zuri la thamani, sisi tunatembelea vifaru na malori,
Unakula chakula kizuri ukipendacho, tunakula wadudu na matunda porini,
Tunakesha ili wewe upate usingizi,
Tunaua ili wewe uishi,
Tunaumia ili wewe upone,
Tunaitoa sadaka "leo yetu" kwa manufaa ya "kesho yako",
Tunatoa sadaka maisha yetu ili kutetea maisha yako,
Tunakupigania usiku na mchana kwa sababu tunakupenda,
Tunaipenda nchi yetu,
Sisi ni wanajeshi,
Sisi ni wazalendo,
Sisi ni mashujaa,
Ombea wote waliofia vitani,
Wamekufa wakitetea nchi yetu,
Wamekufa wakitetea uhai wako,
Ni mashujaa wetu,
Nchi yetu,
Amani yetu,
Jeshi letu.
DEDICATE TO OUR DEFENCE FORCE....
"FOR GOD AND MY COUNTRY" One of the words of the frontline KDF
Tunala na bunduki ili wewe ulale na mwenzi wako,
Tunalala porini ili wewe ulale kwenye nyumba,
Unavaa kofia maridadi ya kupendeza, sisi tunavaa kofia ngumu na nzito za chuma,
Unavaa "vest" nzuri ya pamba, sisi tunavaa "vest" za shaba,
Unavaa mkanda wa ngozi kiunoni, sisi tunavaa mikanda ya risasi,
Asubuhi unaamshwa na "alarm" nzuri ya simu yako, sisi tunaamshwa na milio ya mabomu na risasi,
Unatembelea gari zuri la thamani, sisi tunatembelea vifaru na malori,
Unakula chakula kizuri ukipendacho, tunakula wadudu na matunda porini,
Tunakesha ili wewe upate usingizi,
Tunaua ili wewe uishi,
Tunaumia ili wewe upone,
Tunaitoa sadaka "leo yetu" kwa manufaa ya "kesho yako",
Tunatoa sadaka maisha yetu ili kutetea maisha yako,
Tunakupigania usiku na mchana kwa sababu tunakupenda,
Tunaipenda nchi yetu,
Sisi ni wanajeshi,
Sisi ni wazalendo,
Sisi ni mashujaa,
Ombea wote waliofia vitani,
Wamekufa wakitetea nchi yetu,
Wamekufa wakitetea uhai wako,
Ni mashujaa wetu,
Nchi yetu,
Amani yetu,
Jeshi letu.
DEDICATE TO OUR DEFENCE FORCE....
"FOR GOD AND MY COUNTRY" One of the words of the frontline KDF
Comments