Skip to main content

KTN's investigative journalist Mohamed Ali open letter to the president about the security issue in kenya

KTN's investigative journalist Mohamed Ali wrote the president a letter in Swahili about the security issue in the country.Read the letter below: Rais,Habari ya siku nyingi? Jina langu ni Mohammed Ali, mwandishi wa habari ya runinga ya KTN. Mara ya mwisho kuonana naye ilikua wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu uliopita huko Mombasa katika shule ya msingi ya Khadija. Ulikua mchangamfu kando na ahadi chungunzima kwa Wakenya. Ahadi za tarakilishi za bure kwa wanafunzi wa darasa la kwanza, kutoa nafasi za kazi milioni moja kila mwaka kwa vijana, kuekeza katika usalama wa kitaifa miongoni mwa ahadi zingine. Lakini, kwa hivi sasa bwana rais nahofia ahadi hizo zimekua tasa. Barua yangu inaanza na maswala ya usalama ambayo nimeyapa kipau mbele. Kwanza kabisa nauliza, “Uko wapi? Hatukuoni bwana Rais.” Wakenya wanashabuliwa kila mara na kuuliwa kinyama. Walioponea wamebagi na vilema vya maisha. Shambulizi la Westgate na ahadi ya serikali yako zilionekana kama hekaya za Abunuasi. Uliowapa majukumu ya kutulinda wako wapi? Kuanzia Mkurugenzi wa NIS, Michael Gichangi, Inspekta Jenerali wa Polisi, David Kimaiyo, Mkurugenzi wa CID, Ndegwa Muhoro, Kamanda wa GSU, Kitili Mboya, Waziri wa Usalama wa Ndani, Joseph Ole Lenku na Mkuu wa Majeshi, Julius Waweru Karangi. Ukweli wa mambo ni kwamba Wakenya wanahisi kuwa nyote mmelala. Usalama umegeuzwa na kuwa mchezo wa tufe. Tumejisahau kiasi cha hata kuonyesha siri zetu za ndani kwa maadui zetu. Hatujui tunapigana na nani. Katika kazi yangu ya uandishi wa habari, nimezungumza na wadadisi wa maswala ya usalama na bwana Rais wengi wao wanahisi twapigana wenyewe kwa wenyewe. Na iwapo si wenyewe kwa wenyewe basi twafukuzana na kivuli cha fimbo ambacho hakisitiri jua. Badala ya kuua magaidi tunajiua wenyewe kwa wenyewe. Kwa kweli hatuwezi shinda vita hivi ikiwa twaumizana wenyewe kwa wenyewe badala ya kuungana. Mara tunaambiwa ni MRC, mara ni Mungiki, mara magaidi, maragodoro na sasa waziri wako Ole Lenku ana mapya zaidi. Waswahili wanasema “Bata ata umlishe mawe bado atahara”. Bwana Rais, tumwamini nani? Bwana Rais, majuzi uliingia na taswira mpya kabisa katika uwanja wa Nyayo; magari ya kujikinga na risasi na usalama zaidi. Hii, si kawaida tangu uongozi wa Hayati Mzee Jomo Kenyatta, Daniel Toroitich arap Moi na Mwai Kibaki. Iwapo wewe unahofia, je sisi walalahoi tutahisi vipi? Mauaji ya Mpeketoni ni sawia nay ale ya Tana River. Damu ya wana Mpeketoni inalilia haki. Kina mama wamechwa bila watoto na waume huku watoto wakisalia mayatima kwa kosa la serikali walilolichagua ki katiba, serikali iliyowaahidi kuwalinda pamoja na mali zao. Mauaji ya kiholela yanazidi kugonga vichwa vya habari, baadhi ya walinda usalama wameamua wao ndio majaji na mawakili kwa Wakenya wanyonge wasio na mtetezi. Bwana Rais, wakenya wanalia; kuanzia Easatleigh, Baragoi hadi Mandera. Nina machungu na mengi ya kukueleza lakini muda hauniruhusu. Kumbuka Kenya ni jina, nchi ni sisi. Ni hayo tu kwa sasa. Shukran

Comments

Popular posts from this blog

Take care of yourself__"The first wealth is health".

By Strive Masiyiwa  A few weeks ago I went to the doctor. I will tell you what he said about my health at the end, but first read this: Twenty years ago, I arranged to meet a well-known British international businessman who invested a lot in Africa at the time. We agreed to meet for dinner at a leading hotel in London.  After a good meeting, we started to walk out of the restaurant when he suddenly collapsed in the lobby. There was total pandemonium as they rushed to get medical assistance. Being London, an ambulance arrived in minutes. I jumped in the back with him as paramedics wrestled to keep him alive. He had had a heart attack and had to have triple bypass heart surgery. Sadly he died a few weeks later. He hadn't been sick and his sudden death surprised everyone. And yet as I reflected on it, and later discussed it with a doctor friend who knew him, I realized he was very laid back about his health despite having a hectic business life. Even during our dinner...

The 4 Focuses of History-Makers

kenyabittertruth has given you 200 MB Data. To claim click here https://refer.airtel.africa/KE/F7VT3NZG and download the MyAirtel App using this code: F7VT3NZG “The life given us, by nature is short, but the memory of a well-spent life is eternal.” —Cicero The sunrise was dazzling as the entrepreneur and the artist walked hand-in-hand along the seashore to meet the billionaire at the designated meeting spot for the next morning’s mentoring class. Mr. Riley was already there when they arrived, sitting on the sand, eyes closed in a deep meditation. He was shirtless, wearing camouflage-patterned shorts similar to the ones The Spellbinder styled the day he appeared on the beach and a pair of rubber diving booties with smiley face emojis scattered over them. You would have been more than amused if you saw him in them. An assistant rushed out of the billionaire’s home the instant he raised a hand toward the heavens, displaying the universal victory sign. Three crisp pages of paper were effic...

THE CROWN YOU CARRY: A Letter to My LOVELY Daughter FROM THE HEART OF A MOTHER

My Dearest Daughter, As the sun rises over the hills of Limuru, casting golden rays upon the dew-kissed tea leaves, my heart swells with pride, hope, and the wisdom only a mother can carry. You, my beautiful girl, are in school, and while the world sees a student in uniform, I see a queen in the making. I see the grace of your grandmother, the fire of your ancestors, and the promise of a bright African dawn glowing in your eyes. This Easter, God granted me the sweet joy of bonding with you—not just as a mother—but as a woman who has walked a little further on this winding road of life. You may not know it yet, but in those laughter-filled mornings and quiet evening chats, a legacy was passed on: not of gold or silver, but of values, vision, and virtue. Let me speak to your soul now, daughter of mine. Listen with your spirit. In this life, my sweet child, “a child who does not listen to the mother’s advice will sleep with the flies” — a Ghanaian proverb as old as wisdom itself. The worl...