Skip to main content

KTN's investigative journalist Mohamed Ali open letter to the president about the security issue in kenya

KTN's investigative journalist Mohamed Ali wrote the president a letter in Swahili about the security issue in the country.Read the letter below: Rais,Habari ya siku nyingi? Jina langu ni Mohammed Ali, mwandishi wa habari ya runinga ya KTN. Mara ya mwisho kuonana naye ilikua wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu uliopita huko Mombasa katika shule ya msingi ya Khadija. Ulikua mchangamfu kando na ahadi chungunzima kwa Wakenya. Ahadi za tarakilishi za bure kwa wanafunzi wa darasa la kwanza, kutoa nafasi za kazi milioni moja kila mwaka kwa vijana, kuekeza katika usalama wa kitaifa miongoni mwa ahadi zingine. Lakini, kwa hivi sasa bwana rais nahofia ahadi hizo zimekua tasa. Barua yangu inaanza na maswala ya usalama ambayo nimeyapa kipau mbele. Kwanza kabisa nauliza, “Uko wapi? Hatukuoni bwana Rais.” Wakenya wanashabuliwa kila mara na kuuliwa kinyama. Walioponea wamebagi na vilema vya maisha. Shambulizi la Westgate na ahadi ya serikali yako zilionekana kama hekaya za Abunuasi. Uliowapa majukumu ya kutulinda wako wapi? Kuanzia Mkurugenzi wa NIS, Michael Gichangi, Inspekta Jenerali wa Polisi, David Kimaiyo, Mkurugenzi wa CID, Ndegwa Muhoro, Kamanda wa GSU, Kitili Mboya, Waziri wa Usalama wa Ndani, Joseph Ole Lenku na Mkuu wa Majeshi, Julius Waweru Karangi. Ukweli wa mambo ni kwamba Wakenya wanahisi kuwa nyote mmelala. Usalama umegeuzwa na kuwa mchezo wa tufe. Tumejisahau kiasi cha hata kuonyesha siri zetu za ndani kwa maadui zetu. Hatujui tunapigana na nani. Katika kazi yangu ya uandishi wa habari, nimezungumza na wadadisi wa maswala ya usalama na bwana Rais wengi wao wanahisi twapigana wenyewe kwa wenyewe. Na iwapo si wenyewe kwa wenyewe basi twafukuzana na kivuli cha fimbo ambacho hakisitiri jua. Badala ya kuua magaidi tunajiua wenyewe kwa wenyewe. Kwa kweli hatuwezi shinda vita hivi ikiwa twaumizana wenyewe kwa wenyewe badala ya kuungana. Mara tunaambiwa ni MRC, mara ni Mungiki, mara magaidi, maragodoro na sasa waziri wako Ole Lenku ana mapya zaidi. Waswahili wanasema “Bata ata umlishe mawe bado atahara”. Bwana Rais, tumwamini nani? Bwana Rais, majuzi uliingia na taswira mpya kabisa katika uwanja wa Nyayo; magari ya kujikinga na risasi na usalama zaidi. Hii, si kawaida tangu uongozi wa Hayati Mzee Jomo Kenyatta, Daniel Toroitich arap Moi na Mwai Kibaki. Iwapo wewe unahofia, je sisi walalahoi tutahisi vipi? Mauaji ya Mpeketoni ni sawia nay ale ya Tana River. Damu ya wana Mpeketoni inalilia haki. Kina mama wamechwa bila watoto na waume huku watoto wakisalia mayatima kwa kosa la serikali walilolichagua ki katiba, serikali iliyowaahidi kuwalinda pamoja na mali zao. Mauaji ya kiholela yanazidi kugonga vichwa vya habari, baadhi ya walinda usalama wameamua wao ndio majaji na mawakili kwa Wakenya wanyonge wasio na mtetezi. Bwana Rais, wakenya wanalia; kuanzia Easatleigh, Baragoi hadi Mandera. Nina machungu na mengi ya kukueleza lakini muda hauniruhusu. Kumbuka Kenya ni jina, nchi ni sisi. Ni hayo tu kwa sasa. Shukran

Comments

Popular posts from this blog

Take care of yourself__"The first wealth is health".

By Strive Masiyiwa  A few weeks ago I went to the doctor. I will tell you what he said about my health at the end, but first read this: Twenty years ago, I arranged to meet a well-known British international businessman who invested a lot in Africa at the time. We agreed to meet for dinner at a leading hotel in London.  After a good meeting, we started to walk out of the restaurant when he suddenly collapsed in the lobby. There was total pandemonium as they rushed to get medical assistance. Being London, an ambulance arrived in minutes. I jumped in the back with him as paramedics wrestled to keep him alive. He had had a heart attack and had to have triple bypass heart surgery. Sadly he died a few weeks later. He hadn't been sick and his sudden death surprised everyone. And yet as I reflected on it, and later discussed it with a doctor friend who knew him, I realized he was very laid back about his health despite having a hectic business life. Even during our dinner...

WHERE TO BUY THINGS AT A BARGAIN IN NAIROBI

 1.Cereals – Get them in Nyamakima in that kichochoro for Molo matatus. Groundnuts from the market cost Sh190 per kilo, but at Nyamakima they are Sh110. You can also get apples and other fruits at a good price. 2.  Diapers and bar soap – OTC. The kichochoro between Tuskys and Equity.  3. Chemicals for homemade detergent, bleach, fabric softener, disinfectant – OTC, the building with Tuskys, go upstairs, first floor. They will even explain how to mix them.  4. Bulk shopping – If you can manage to go to Kawangware or Eastleigh, you will save a lot. In Kawangware, go to Samrose in the market. Alight at Mlango Soko, then at Cooperative Bank, go down and turn at the first right turn, walk about 20 metres and you will find SamRose. Go with a list, they will give you the prices. If you are buying things for a shop, they deliver. Alternatively, you can turn left and walk a bit for like 100 metres where you will find many wholesale shops including FairPrice. Also look out for Israel. In Eastlei...